Blog smart kwa kutumia Microsoft word

Mwandishi Hemedans Nassor

Kuna watu wengi wanamiliki blogs Tanzania lakini hawana uwezo wa kucode na kusababisha kupata shida sana wanapotaka kucostomize post za blog ziwe kama wanavyotaka wao. Lakini watu hao hao unakuta ana uwezo mkubwa tu wa kutumia Microsoft word. Leo nitawaelekeza namna ya kuitumia Microsoft word kupost kwenye blog yako. Njia hii itawanufaisha wanoblog kwa blogspot na wordpress.

 

Vitu vilivyomo kwenye Microsoft word vitakavyokunufaisha

032313 2045 blogsmartkw1

  1. Uwezo wa kuangalia homepage ya blog yako kupitia Microsoft word (itafungua kwa browser)
  2. Unaweza kuieka post ya blog yako katika category yoyote uliyotengeneza kupitia Microsoft word
  3. Unaweza kuedit post ya zamani kupitia Microsoft word
  4. Unaweza kueka account mbali mbali kwenye Microsoft word yako kwa ajili ya kublog
  5. Kupublish blog post kutokea Microsoft word

 

NJIA ZA KUFATA ILI KUWEZA KUBLOG NA MICROSOFT WORD

 

Step ya kwanza

Andika post yako kwenye Microsoft word kama unavyoandika kazi nyengine remba kadri unavyoweza, ukitaka weka picha idadi unayotaka hadi post ikamilike.

Step ya pili

Bonyeza file then bonyeza save and send then bonyeza publish as a blog post (hii ni kwa Microsoft word 2010) kwa wanaotumia Microsoft 2007 njia inaweza kua tofauti kidogo ila lengo ni moja.

032313 2045 blogsmartkw2

 

Step ya tatu

Itafunguka sehemu nyengine click publish as a blog post

032313 2045 blogsmartkw3

 

Step ya nne

Itafunguka sehemu ya blog eka title na kama unataka kuieka post kwenye category Fulani utaeka hapa, kama ni mara ya kwanza kutumia itabidi uset username na password ya acont yako ya blog hapa. Then utapublish 4

 

JINSI YA KUSET USERNAME NA PASSWORD

Kama ni mara ya kwanza ukiclick publish itapop up sehemu ya kueka username na password lakini kama ni mtumiaji tayari click manage account then add.

032313 2045 blogsmartkw4

Mara yako ya kwanza utaambiwa uchague provider wako wa blog. Kuna kina blogspot, wordpress, typepad, community server, sharepoint blog na windows live space. Utachagua kutokana na provider wa blog unaetumia. Mfano mimi nimechagua wordpress.

032313 2045 blogsmartkw5

Hio sehemu nilipozungushia red utaeka url ya blog yako hapo utaondoa <enter your blog URL here > na utareplace url yako. Mfano mi na assume url yangu inaitwa blogyangu.wordpress.com

032313 2045 blogsmartkw6

Then unaeka user na password ur done. Enjoy kublog.

 

kumbuka Picha zinakua uploaded automatic so usihofie na pia kama unataka kuadd feature image publish kama draft kwa ajili ya kuadd badae

Avatar of hemedans nassor
Mwandishi Hemedans Nassor Mchangiaji
Hemedans aka Chief Mkwawa, amekuwa mwandishi wa makala mbalimbali za teknolojia kuanzia kuanzishwa kwa Mtaawasaba. Kwa sasa ni mchangiaji kila anapopata nafasi
2 Comments

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive