Samsung Max: Programu mpya ya Android ya usimamizi na ufuatiliaji wa matumizi ya data.

Mwandishi Diana Benedict

Leo Samsung imezindua Proramu ya mfumo endeshi wa Android ambayo itamsaidia mtumiaji wake, kudhibiti matumizi ya Data, kutoa ulinzi na kuzuia uhalifu wa mtandao kwenye Simu yako. Kabla ya Samsung Max ilikuwa programu ya Opera Max ambayo imebadilishwa na kuwa Samsung Max.

Samsung

Kwa Samsung Max, watumiaji wanaweza kudhibiti matumizi yao ya data na kunufaika na vipengee vya faragha vyema kwa bure kabisa.
Samsung Electronics leo imezisha Programu ya Samsung Max, programu mpya na ya bure ya Android iliyoundwa ili kukuza usimamizi wa data za simu za mkononi na usimamizi wa faragha (Privacy Protection), na ufuatiliaji wa matumizi ya data na usalama wa Wi-Fi umeboreshwa zaidi. Kuanzia leo hii Februari 23, 2018 programu itakuwa inapatikana kwa kupakuliwa kwenye Google Play. Samsung Max itasaidia vipengele vipya vya kipekee na rahisi vya kutumia Samsung, ‘Data Saving Mode’ na ‘Ulinzi wa Faragha (Privacy Protection).’ Samsung Max inakuja badala Opera Max – mojawapo ya mtandao wa faragha ya binafsi za simu za mkononi (Mobile Virtual Private Networks (VPNs) duniani – na sasa inapatikana kwa mamilioni ya watumiaji zaidi hasa wa Samsung.

“Kote duniani, data imekuwa ikitumika sana, lakini mipango mingi bado ni ghali kwa watumiaji ambao wanataka kupata teknolojia ya kisasa zaidi katika vifaa vyao,” alisema Seounghoon Oh, Makamu wa Rais wa Samsung R & D Institute India.  “Kwa Samsung Max, watumiaji wetu katika kila kona ya dunia sasa imeongeza uhuru na udhibiti juu ya matumizi yao ya data na faragha hasa wakati huu wa ulio ongezeka kwa vitisho vya usalama programu za udanganyifu na maelezo ya mtumiaji.” Aliongeza

Tuangazie Programu hii imelenga vipengele vipi kwa mtumiaji

Njia ya Kuokoa Data – Hali ya Kuhifadhi data inayofanya mpangilio wa data kufanya kazi kwa bidii na kwenda zaidi. Katika hali nyingine, inaweza kutumika hata kukusaidia kuokoa fedha kwenye mpango wako wa data ya simu kupitia mtoa huduma wako wa data. Kipengele hiki hutoa ushauri smart juu ya matumizi ya data..
Njia ya Ulinzi wa Faragha – Katika Maeneo ya Wi-Fi ya wazi (open Wi-Fi) utalindwa na encryption ya kuzuia tracker. Vipengele hivi pia hutoa faida za faragha kwenye mitandao ya simu, ambayo inaruhusu Samsung Max kutoa ulinzi wa faragha kwenye Data ya Simu ya Mkononi au Wi-Fi kwenye programu zako zote. Hii inaruhusu watumiaji kupata usalama kwa intaneti kwa watumiaji.
Upatikanaji
Samsung Max itakuja preloaded kwenye smartphones zote za Samsung zitakazotoka kuanzia sasa hasa Galaxy A na Galaxy J nchi za India, Argentina, Brazil, Indonesia, Mexico, Nigeria, Afrika Kusini, Kenya, Tanzania, Thailand na Vietnam. Watumiaji wengine wataweza kushusha Samsung Max kwenye vifaa vingine vya Samsung na Adnroid Device yoyote kupitia Google Play Store au Galaxy Apps.

2000px get it on google play. Svg

Watumiaji wa Samsung ambao kwa sasa wanatumia programu ya Opera Max, watapata maboresho moja kwa moja ya Samsung Max kuanzia Februari 23, 2018.

Endelea kuwa nasi kwa kutufuata kwenye mitandao ya kijamii, na usisahau ku subscribe ili uwe wa kwanza kupata Habari, Uchambuzi na Makala mbali mbali za kisayansi na teknolojia. Pia usisahau ku acha maoni yako hapo chini na unaweza kuwasiliana nasi kwa barua pepe mhariri@mtaawasaba.com

 

Avatar of diana benedict
Mwandishi Diana Benedict Mwandishi
Mitandao ya Kijamii
Diana Benedict. Digital Creator | IT Specialist | Graphics Designer | Web Designer | Web SEO | Contents Management | UI/UX Designer and Social Media Management.
Maoni yako

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive