MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Tovuti 5 za kutembelea kama unatafuta ajira Tanzania (2023)
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Chaguo la Mhariri > Tovuti 5 za kutembelea kama unatafuta ajira Tanzania (2023)

Tovuti 5 za kutembelea kama unatafuta ajira Tanzania (2023)

Imeandikwa na Emmanuel Tadayo Mwaka 1 uliopita
Sambaza
ajira Tanzania 2022
Yaliyomo
Ajira LeoAjira yakoAjira zetuBrighter  Monday (Zoom Tanzania Jobs)EmpowerJobs Today (Tanzania)MabumbeUdahili PortalHitimisho
Changamoto ya upatikanaji wa Ajira Tanzania 2022 imekuwa kubwa ukilinganisha na miaka ya nyuma, hivyo zoezi la kutembea na bahasha ya khaki kutoka ofisi moja hadi ingine imekuwa ni changamoto kubwa ingine.

Hapa ndio unapokuja umuhimu wa tovuti za ajira Tanzania, Tovuti hizi zinakuleta mtafutaji wa ajira karibu na waajiri mbalimbali kuanzia mashirika binafsi, taasisi za serikali na kadhalika na kurahisisha zoezi zima la utafutaji ajira.

Kama unatafuta ajira Tanzania 2022, kuna tovuti nyingi ambazo zimejikita katika kuunganisha watafuta ajira na waajiri ambazo zitakusaidia kutafuta ajira kutokana na utaalamu na uzoefu wako.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Starlink kuanza kutoa huduma za intaneti Tanzania robo ya kwanza 2023

Makala hii inakuletea tovuti 5 za ajira Tanzania 2022 ambazo ni za uhakika katika kukusaidia kukukutanisha na waajiri mbalimbali.

Ajira Leo

Tovuti hii huchapisha nafasi mpya za ajira kila siku kutoka kwa waajiri mbalimbali nchini, Pia tovuti hii huchapisha nafasi za scholarships kutoka nchi mbalimbali, nafasi za internship pamoja na admission za vyuo mbalimbali nchini. Kama wewe ni mtafutaji wa ajira na unataka ajira kwa haraka basi hakikisha unatembela tovuti hii kila siku.

Ajira yako

Tovuti hii hukuleta karibu mtafutaji wa ajira na waajiri mbalimbali ikiwemo makampuni mbalimbali nchini Tanzania Pamoja na taasisi za ki serikali na zile zisizo za serikali. Nafasi za ajira hutangazwa kila siku hivyo kuleta urahisi wa kujua kazi husika imetangazwa lini, na kama muda wa tangazo hilo umeisha au la. Cha kufurahisha ni kwamba matangazo haya ya ajira ni bure kabisa na usikubali kulipa mtu yoyote ili kupata nafasi za ajira zinazotangazwa kwenye tovuti hii ya Ajira Yako

Ajira zetu

Tovuti hii inafanana kwa namna nyingi na hizo juu, ambapo tovuti hii itakuwezesha kutafuta ajira kutoka makampuni na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali ambazo  hutangaza nafasi za ajira kila siku kupitia tovuti hii. Pia ikiwa mtu ana maswali kuhusu jambo lolote, baada ya kufungua tovuti hiyo huwa kuna ujumbe unakuja ambao humuwezesha mtu kuuliza na kujibiwa maswali moja kwa moja mara baada ya kuandika jina na barua pepe yake.

Brighter  Monday (Zoom Tanzania Jobs)

Tovuti hii ni moja ya tovuti kubwa na ni bure kabisa kwa watafuta ajira, itakukutanisha na waajiri mbalimbali ikiwemo mashirika na makampuni ya binafsi. Tovuti hii itakutaka kutengeneza profile ambayo utaweka taarifa zako ikiwemo CV na taarifa zako za elimu, ujuzi wako na machaguo mengine kuhusu ajira unayohitaji. Utakuwa ukipokea ujumbe kwa njia ya barua pepe kila nafasi ya ajira inayofanana na vigezo vyako inapochapishwa.  Pia tovuti hii huchapisha ushauri, mbina na mengine mengi kuhusu ajira na utafutaji wa ajira kwa ujumla

Empower

Tovuti hii inafanana kwa kiasi kikubwa na Brightermonday. Tovuti hii itakutaka kutengeneza profile ambayo utaweka taarifa zako ikiwemo CV na taarifa zako za elimu, ujuzi wako na machaguo mengine kuhusu ajira unayohitaji. Utakuwa ukipokea ujumbe kwa njia ya barua pepe kila nafasi ya ajira inayofanana na vigezo vyako inapochapishwa.  Pia tovuti hii huchapisha ushauri, mbina na mengine mengi kuhusu ajira na utafutaji wa ajira kwa ujumla

Pia unaweza tembelea hizi;

Jobs Today (Tanzania)

Jobs Today ni tovuti nyingine ambayo ni bora kwa ajili ya kufauta nafasi za kazi hapa nchini Tanzania, tovuti hii ni kama tovuti nyingie zilizo tangaulia lakini hii ina angazia zaidi kwenye mchanganyiko wa ajira pamoja na elimu kwa nchini Tanzania. Kupitia tovuti hii hutaweza kuangalia nafasi mpya za kazi kila siku, pamoja na nafasi za scholarships, na admission.

Mabumbe

Tovuti hii inakuletea nafasi za ajira kutoka nchini Tanzania na nchi zingine za Jirani kama Kenya na Zambia kila siku, pia wanakuletea nafasi za scholarship kutoka nchi mbalimbali.

Udahili Portal

Udahili Portal ni tovuti nyingine ambayo ni bora kwa ajili ya kufauta nafasi za kazi hapa nchini Tanzania, tovuti hii ni kama tovuti nyingie zilizo tangaulia lakini hii ina angazia zaidi kwenye mchanganyiko wa ajira pamoja na elimu kwa nchini Tanzania. Kupitia tovuti hii hutaweza kuangalia nafasi mpya za kazi kila siku, pamoja na nafasi za scholarships, na admission.

Hitimisho

Kupitia mtandao wa intaneti  wengi wamepata ajira rasmi na zisizo rasmi. Hivyo ni muhimu kupitia tovuti, blogu, mitandao ya kijamii kama instagram, facebook, LinkedIn na kadhalika ili kuweza kupata kazi ambayo unaweza kuimudu kulingana na ujuzi na utaalamu ulio nao.

Pia ni vyema kwa muombaji wa ajira kuwa na nyaraka muhimu zinazoweza kuhitajika kwa haraka kama vile kitambulisho cha kitaifa kinachotolewa na NIDA, na vyeti vya kuhitimu masomo au ujuzi mbalimbali alionao muhusika ili kurahisisha mchakato wa uombaji ajira katika taasisi,mashirika na kampuni mbalimbali kwa urahisi.

Mtaawasaba inakutakia utafutaji mwema wa ajira kupitia mtandao wa intaneti. Pia usisahau kutembelea mitandao yetu ya kijamii instagram, twitter na Facebook, pia tembelea na utufuate kwenye channeli yetu ya YouTube

KWENYE Ajira
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Maoni 6
  • Avatar of Vianey mgarula Vianey mgarula anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 19:53

    To tovuti yenu ni mhimu kuna wengi imewasaidia

    Jibu
  • Avatar of Roman R. Leka Roman R. Leka anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 11:24

    Nashukuru sana nimepata maarifa ya ziada kupitia chapisho lako hapo juu, ninaenda kupitia kila moja kuona fursa inayopatikana kulingana na taaluma yangu ya Uhasibu.
    Nakutakia Ufanisi mwema ktk majukumu ya ujenzi wa taifa.

    Jibu
  • Avatar of Sadi juma mzugi Sadi juma mzugi anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 07:20

    Nitafulahi kama nitapata taarifa majibu yatakapo tolewa

    Jibu
  • Avatar of Sadi juma mzugi Sadi juma mzugi anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 07:18

    Maombi ya ajira ya udereva

    Jibu
  • Avatar of Khamis Nassor khamis Khamis Nassor khamis anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 06:46

    Mim natafuta ajira nina elimu ya afisa habibi diploma

    Jibu
  • Avatar of Emmanuel vundwe Emmanuel vundwe anasema:
    Mwezi 1 uliopita kwa 06:42

    Natafta kazi ya udelewa mkoa wa mbeya 0765689910

    Jibu

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?