MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Habari > Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Imeandikwa na Amos Michael Siku 4 zilizopita
Sambaza
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Leo tarehe 16, Februari 2023 kampuni ya huduma za mawasiliano ya Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania kwa wateja wake. eSIM (SIM iliyopachikwa) – ni mfumo wa kidijitali unaomuwezesha mtumiaji wa simu kupata huduma za mawasiliano bila kupachika laini kwenye simu. Unaweza kusoma zaidi kuhusu mfumo huu wa eSIM hapa.

Kupitia huduma hii, wateja wa Airtel wanaweza kusajili zaidi ya laini moja kwenye akaunti moja. Hii inamaanisha kwamba wateja wanaweza kuwa na simu mbili kwenye akaunti moja bila ya kuhitaji kadi ya SIM kwa kila simu.

Unaweza Kusoma

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Starlink kuanza kutoa huduma za intaneti Tanzania robo ya kwanza 2023

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano alisema kuwa Airtel imefungua njia kwa kuwa mtoa huduma wa kwanza wa eSIM nchini Tanzania. Ameyasema haya leo jijini Dar es Salaam kwenye hafla ya uzindduzi wa huduma hii,

Kulingana naye kampuni hiyo imekuwa ikiwekeza katika bidhaa na huduma za ubunifu zinazoendana na maisha ya kila siku ya kidijitali ya wateja wetu na uzinduzi wa eSIM ni ushuhuda wa dhamira yao kwa Tanzania.

Akifafanua zaidi, Bi. Singano aliongeza kusema kuwa huduma ya eSIM kwa sasa inapatikana kwenye mtandao wa Airtel na wateja wanaotaka kubadili kadi zao za sasa za SIM kwenda eSIM watahitaji kutembelea Duka lolote la Airtel nchini na kuongozwa kubadilishana SIM zao kwenda eSIM.

Wateja wanaweza pia kuongeza nambari mpya kwenye eSIM, wakati wanaendelea kutumia SIM za kawaida. Kwa kuwa na eSIM kutoka Airtel Tanzania, hawahitaji tena kuwa na simu kadhaa ili kubeba sim kadi na wanaweza kutumia hadi namba tano kwa simu moja.

Sio simu zote zinaweza kupata huduma hii ya eSIM. Kama wewe ni mteja wa Airtel Tanzania, unaweza kupiga *#06# ili kuona kama simu yako ina uwezo wa kutumia eSIM. Kuhusu kupiga *#06# kwa simu zinazooana namba ya EID itaonyeshwa’, akifafanua zaidi Singano amesema kuwa kadi ya eSIM haiwezi kuondolewa au kuibiwa, wakati kadi za SIM kawaida zinazoweza kutolewa wakati mwingine huibiwa, na kutumika katika utapeli hivyo usalama wa hali ya juu.

Msanii wa kizazi kipya, Diamond Platnumz ambaye alikuwepo kwenye uzinduzi wa huduma hii mpya na ya kwanza Tanzania, ameipongeza Airtel kwa kuzindua huduma hii nchini. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond ameonesha furaha yake kwa hatua hii ya kisasa na kuwahimiza wateja wa Airtel kuitumia huduma hii mpya.

Nini maoni yako kuhusu huduma hii mpya kutoka Airtel Tanzania? Tujulishe kwenye comment section hapo chini.

 

KWENYE Airtel Tanzania, eSim
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 3 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita
Sasa unaweza kujitumia ujumbe kupitia WhatsApp

Sasa watumiaji wa Android na iOS wanaweza kujitumia ujumbe kupitia WhatsApp

Miezi 4 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?