MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma BasiGo imekusanya dola milioni 6.6 kuleta mabasi ya umeme Kenya
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Magari > BasiGo imekusanya dola milioni 6.6 kuleta mabasi ya umeme Kenya

BasiGo imekusanya dola milioni 6.6 kuleta mabasi ya umeme Kenya

Imeandikwa na Emmanuel Tadayo Miezi 4 iliyopita
Sambaza
Kampuni ya BasiGo imekusanya dola milioni 6.6 za ufadhili kuleta huduma ya mabasi ya umeme Kenya

Kampuni inayojihusisha na utengenezaji wa magari ya umeme ya BasiGo, inayofanya shuguli zake nchini Kenya, imekusanya takribani dola za kimarekani milioni 6.6 kuleta mabasi yanayotumia umeme yatakayotumika kwa ajili ya usafiri wa umma nchini Kenya. Kiasi icho kimepatikana kutoka Toyota, kupitia kampuni yake tanzu ya ubia ya Mobility 54.

Toyota ilitoa kiasi cha dola za Marekani milioni 1 kwenye mradi wa BasiGo. Wawekezaji wengine walioshiriki ni pamoja na Novastar; kampuni ya VC inayolenga Afrika na Trucks.vc, kampuni ya VC yenye makao yake Silicon-Valley ambayo inaunga mkono startups katika sekta ya usafirishaji.

Fedha hizi zinatarajiwa kutumika katika kuharakisha juhudi za BasiGo kutengeneza mabasi ya umeme kwa ajili ya usafiri wa umma nchini Kenya na bara la Afrika kwa ujumla.

Toyota imekuwa ikifadhili startups zinazojihusisisha na umeme, baadhi ikiwa ni pamoja na Zembo, mtengenezaji wa pikipiki ya umeme nchini Uganda, na Aceleron mtengenezaji wa betri wa Uingereza.

Inasemekana, mabasi 15 ya umeme ya BasiGo yatawasilishwa mwezi januari 2023 na yataanza kufanya kazi na waendeshaji wengi wakubwa wa mabasi jijini Nairobi.  Kampuni hii inatarajiwa kuweka kuweka miundombinu rahisi zaidi ya kuchaji kote nchini katika kipindi chote cha mwaka 2023. Pia, kampuni hiyo inasema, kuwa inatarajia kuwa na mabasi zaidi ya 1000 ya umeme yanayofanya kazi nchini Kenya ifikapo 2025.

BasiGo itatoa mabasi ya umeme kwa waendeshaji wakubwa wa mabasi nchini Kenya kupitia suluhisho la kipekee la ufadhili wa kampuni ya “Pay-As-You-Drive”, ambalo linawawezesha wamiliki wa mabasi ya umma kununua basi la umeme kwa gharama sawa na basi sawa la dizeli.

 

KWENYE BasiGo
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Ramani, Kampuni kutoka Tanzania yakusanya $32m

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Miezi 4 iliyopita
NALA yakusanya bilioni 23.1

Kampuni ya huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji

Mwaka 1 uliopita
Kutana na Gari la kujiendesha lenyewe lisilo na usukani

Kutana na Gari la kujiendesha lenyewe lisilo na usukani

Miaka 5 iliyopita
One litre car

One litre car: Gari linalotembea kilomita 100 kwa lita moja tu.

Miaka 10 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?