MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Kampuni ya huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Chaguo la Mhariri > Kampuni ya huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji

Kampuni ya huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji

Imeandikwa na Emmanuel Tadayo Mwaka 1 uliopita
Sambaza
NALA yakusanya bilioni 23.1
Kampuni ya kitanzania inayotoa huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji.

Fedha hiyo ambayo ni sawa na dola za kimarekani milioni 10 imekusanywa kutoka kwa wawekezaji wakiwemo Amplo, Accel, na washirika wa Bessemer, pia kwa ushirikiano na wachangiaji wengine wakiwemo waanzilishi wa kampuni za Monzo, Robinhood, Alloy na Deel. Pia NALA inatarajiwa kuanzisha kampeni ya uchangiwaji mwaka huu na watumiaji wa mwanzo wataweza kumiliki hisa kwenye kampuni ya NALA.

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali, kampuni ya NALA imepanua wigo wa utoaji huduma za kutuma na kupokea fedha ambapo mwanzoni ilikuwa ni ndani ya nchi tu, sasa itawezesha kutuma na kupokea fedha kutoka Uingereza kwenda nchi kadhaa za Afrika ikiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Ghana. Kwa mujibu wa NALA, takribani watumiaji 8000 wamefanya miamala yenye thamani zaidi ya dola za kimarekani millioni 10 kwenda nchi kadhaa za Afrika ndani ya miezi sita iliyopita.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Afrika ni moja ya maeneo ambayo ni ghali sana kutuma na kupokea fedha, kwa gharama za wastani wa asilimia 10.6, watoa huduma zakifedha za kidijitali kama NALA wanatamba kwa wateja wao kama watoa huduma wenye viwango vya chini kabisa vya kutuma na kupokea fedha, wameripoti TechCrunch.

Kufuatia makusanyo haya, NALA inatarajia kutanua huduma zake na kufikia nchi 12 za kiafrika ikiwemo Nigeria mpaka kufikia mwisho wa mwaka huu, pia inatarajia kuzindua huduma za kuhamisha fedha Marekani na nchi za ulaya ndani ya robo ya kwanza.

Akiongea na gazeti la The Citizen, Mkurugenzi mtendaji bwana Benjamin Fernandes alisema NALA itatumia fedha hizi kuboresha miundombinu ili kurahisisha huduma zao, ” Naamini huduma za malipo kwenye bara la afrika zimetengenezwa kwa asilimia 1, tunahitaji teknolojia sahihi kuhakikisha miundombinu inasimikwa ili kuwezesha mifumo ya huduma za kifedha barani afrika”.

Kwa sasa takribani asilimia 80 ya fedha zinazotumwa Afrika hutumwa kwa njia ya fedha taslimu, na asilimia 20 iliyobaki ndio pekee huamishwa kwa kupitia mikondo ya kidijitali ambayo hata hivyo hukumbwa na changamoto nyingi ikiwemo gharama kubwa za makato kwenye huduma hizo.

KWENYE NALA
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?