MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Chaguo la Mhariri > Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 5 iliyopita
Sambaza
Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Takwimu zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) katika ripoti za robo ya nne ya mwaka inayoishia Desemba 2017 inaonesha ongezeko kubwa la watumiaji wa huduma ya Intaneti kufikia asilimia 45 ya watanzania ambayo ni sawa na watu milioni 23 ukilinganisha na watanzania milioni 7.52 ambao ni sawa na asilimia 12 tu ya watanzania mwaka 2012.

Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Ongezeko la watumiaji linaonesha kwa mwaka 2013 kulikuwa na watumiaji milioni 9.31 sawa na asilimia 21 ya watanzania wote, idadi ya watumiaji iliendelea kupanda kufikia watanzania milioni 12.27 sawa na asilimia 29 ya watanzania wote kwa mwaka 2014. Idadi imezidi kuongezeka mwaka hadi mwaka kama inavoonekana kwenye kielelezo hapo chini.

Mwaka Idadi ya watumiaji Asilimia (ya watanzania)
2012 milioni 7.52 12
2013 milioni 9.31 21
2014 milioni 12.27 29
2015 milioni 17.62 34
2016 milioni 19.86 40
2017 milioni 23 45

 

Katika ripoti ya mwaka 2018 ya Shirika la Kimataifa la Mawasiliano (ITU) yenye jina “Achieving universal and affordable internet in the least developed countries’ iliyotolewa mwishoni mwa mwezi Januari inaeleza kuwa jitihada za kuboresha sera zinazohusu Tehama na uwekezaji katika mkongo wa Taifa wa mawasiliano (NICTBB) ni baadhi ya mambo yaliyofanya Tanzania ifanikiwe kuchochea ukuaji wa matumizi ya intaneti. Ambapo Tanzania ilikopa Dola za Marekani milioni 170 (zaidi ya Sh377 bilioni) kwa awamu mbili kutoka benki ya Exim ya China ili kugharamia mkongo huo wa taifa wa mawasiliano uliosambaa nchi nzima.

Kasi ya ukuaji wa intaneti ni moja ya hatua muhimu ya Tanzania katika kufikia malengo ya ukuaji wa uchumi

Kasi ya ukuaji wa intaneti ni moja ya hatua muhimu ya Tanzania katika kufikia malengo ya ukuaji wa uchumi kwa kutumia Tehama ifikapo mwaka 2020 kama ilivyobainishwa katika lengo namba 9.c la Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa.

Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Pia katika ripoti hii iliyotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)  inaonesha kuwa idadi ya watumiaji wa simu za mkononi imeongezeka na kufikia watumiaji milioni 40 kutoka watumiaji milioni 27.62 kwa mwaka 2012,  mtandao wa simu wa Vodacom Tanzania ukiongoza kwa kuwa na watumiaji waliojisajiliwa 12,714,297 wakifuatiwa na Tigo kwa kuwa na watumiaji waliosajiliwa 11,062,852.

Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23

Katika taarifa hiyo inaonesha aina ya intaneti inayotumika kama simu za mkononi, watumiaji wa intaneti inayohamishika ni takribani watu 19,006,223 huku watumiaji takribani milioni 3.47 wanatumia intaneti ya ‘wireless’ isiyohamishika na watumiaji wapatao 520,698 wanatumia ‘wired internet’ isiyohamishika .

Ripoti: Tanzania yafikisha watumiaji wa Intaneti milioni 23Unaonaje kuhusu takwimu hizi na ongezeka hili la watumiaji wa intaneti Tanzania? Tuandikie maoni yako kwenye sehemu ya kuacha maoni. Pia usisite kutufuata kwenye mitandao ya kijamii kama Fecebook, instagram na Twitter.

KWENYE intaneti, TCRA
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?