Simu isiyoingia maji ya Sony Xperia Z

Mwandishi Alexander Nkwabi

Habari njema kwa watu wote, kampuni ya sony wamezindua simu isiyoingia maji, simu iliyopewa jina la Sony Xperia Z inaweza kuzamishwa mpaka futi 3 chini ya maji kwa muda wa mpaka nusu saa bila kuharibika

Watengenezaji wake waliijaribu bafuni, simu zingine kama iphone huaribika haraka iwapo zitaingia maji au kudondoshwa. Sony Xperia Z imefunikwa kwa kioo kinachokunjika na kuzuia kuvunjika, lakini chembamba kwa milimita 7.9
simu hiyo ilizinduliwa kwenye Consumer Electronics Show (CES) huko Las Vegas,

Sony Xperia Z

simu hiyo pia ina kamera ya hali ya juu yenye – 13 megapixels, yenye nguvu kuliko ile ya iPhone 5 ambayo ni 8 megapixel pekee.

simu hiyo inayotumia android, ina uwezo kuongeza maisha ya betri kwa kuzima programu zisikuwa na umuhimu kwa wakati huo.
pia ina mfumo wa intanet wa 4G connection,na inchi 5 Full HD 1080p.

jiunge nasi kupitia youtube channel yetu

Mwandishi Alexander Nkwabi Mhariri
Mitandao ya Kijamii
Alex ni mhariri mwandamizi hapa Mtaawasaba.com, kwa kipindi kirefu amekuwa akivutiwa na mfumo endeshi wa Android na michezo ya kompyuta. Alex akiwa haandiki hapa Mtaawasaba basi hupendelea kupiga picha, kusafiri na kusoma vitabu.
2 Comments

Trending on Mtaawasaba

Receive Mtaawasaba notifications Click ‘Receive,’ then ‘Allow’ when prompted. Dismiss Receive