MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Spotify yazindua huduma zake Afrika, yaanza na Afrika Kusini
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Habari > Spotify yazindua huduma zake Afrika, yaanza na Afrika Kusini

Spotify yazindua huduma zake Afrika, yaanza na Afrika Kusini

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 5 iliyopita
Sambaza
spotify

Kampuni kubwa kabisa ya ku stream muziki duniani ya Spotify imezindua huduma zake Afrika jumanne hii ambapo kwa kuanzia imezindua huduma zake jijini Johanessburg nchini Afrika Kusini.

Huduma iliyozinduliwa inampa mtumiaji siku 30 za kujaribu huduma ya kulipia ambapo baada ya hapo mtumiaji atarudishwa kwenye huduma yenye matangazo ndani yake au atatakiwa alipie rand 60 ili aendelee kupata huduma bila matangazo ya biashara.

Kampuni hii kutoka Sweden ilizinduliwa mwaka 2008 na huduma zake zimekuwa zikipatikana kwenye mataifa takribani 60 duniani kote, na kwa sasa ndio kampuni kubwa kabisa ya ku stream muziki ikiwa na watumiaji takribani milioni 200 bila kujumuisha Afrika ambako huduma zake zilikuwa hazijaanza kupatikana rasmi.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Starlink kuanza kutoa huduma za intaneti Tanzania robo ya kwanza 2023

Spotify inatarajia upinzani mkubwa kutoka kwa huduma zingine ambazo tayari zinapatikana  Afrika kwa ujumla hasa nchini Afrika kusini zikiwemo Apple Music, Google Play Music, Simfy Africa na Deezer ambazo zinapatikana nchi nyingi za afrika kwa sasa bila kusahau huduma za ku stream zinazotolewa na baadhi ya makampuni ya simu .

Watumiaji wa Afrika kusini hawatahitaji tena kutumia VPN ili kupata huduma za Spotify japo watumiaji wengine wa nchi zilizobaki za Afrika itabidi waendelee kutumia VPN ili kufaidi Spotify.

Sababu kubwa iliyowafanya Spotify kuchelewa kuleta huduma Afrika ni kasi ndogo ya intaneti kwa nchi nyingi za kiafrika na gharama kuwa kubwa kwa bando za intaneti. Kwa utafiti wao wameona Afrika kusini inafaa kuanzia kwa sababu wana intaneti yenye kazi nzuri na huduma za WI-FI zimesambaa maeneo mengi ukilinganisha na nchi zingine barani humo. Huduma za Spotify nchi Afrika kusini zita stream kwa kasi ya 24kbps na inaweza badilika kutokana na kasi ya intaneti itakayopatikana wakati wa kutumia hasa kwenye maeneo yenye mitandao yenye kasi kubwa.

Uzinduzi huu nchini Afrika kusini umekuja wakati Spotify ikijiandaa kuweka hisa zake kwenye soko la hisa la New York, ambapo itaruhusu wawekezaji na wafanyakazi kuuza hisa zao bila kuhitaji kukuza mtaji.

Akizungumza na waandishi wa Reuters, mkurugenzi mtendaji wa Spotify upande wa  mashariki ya kati na Afrika bwana Claudius Boller alisema “Tunaamini Afrika kusini ni nchi nzuri kwa kuanzia” .

Tunaamini Afrika kusini ni nchi nzuri kwa kuanzia

akaongeza “Tumeangalia ukuaji wa teknolojia na hali nchini Afrika kusini tumeona ni soko zuri la muziki na muhimu duniani”

Bwana Claudius Boller amasema pia wana mpango wa kupanua wigo kwa nchi zingine za afrika japo hakuzitaja ni nchi zipi zinazofuata wala ni lini nchi zaidi zitaongezeka.

KWENYE Spotify
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Wiki 1 iliyopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Wiki 2 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?