MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Tweet ya Kylie Jenner yagharimu SnapChat Dola bilioni 1.3
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Apps > Tweet ya Kylie Jenner yagharimu SnapChat Dola bilioni 1.3

Tweet ya Kylie Jenner yagharimu SnapChat Dola bilioni 1.3

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 5 iliyopita
Sambaza
snapchat

Siku ya alhmisi ilikuwa mbaya baada ya hisa za Snapchat kuporomoka ghafla na kampuni iyo imepoteza karibu dola za kimarekani billioni 1.3 mpaka 1.6 kwenye soko la hisa baada ya mwanadada Kylie Jenner ambaye ni  maarufu kwenye reality show ya Keeping Up With The Kardashians, kuandika tweet inayosema hatumii tena mtandao wa kijamii wa Snapchat.

sooo does anyone else not open Snapchat anymore? Or is it just me… ugh this is so sad.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

— Kylie Jenner (@KylieJenner) February 21, 2018

Kylie Jenner ambae akaunti yake ya Snapchat ndiyo inayotazamwa kuliko zingine zote, ni mmoja wa watu mashuhuri wenye ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.Kilichomfanya aandike hivyo ni baada ya kutofurahishwa na mabadiliko makubwa ya muonekano wa SnapChat ambao umelalamikiwa na watumiaji kuwa mgumu kutumia.

Snapchat ambayo kwa sasa inakumbwa na ushindani mkubwa kutoka kwa App zingine za mitandao ya kijamii inayohusisha kushea picha kama Instagram.

Sio Kylie Jenner pekee ambaye amelalamikia mabadiliko ya muonekano bali, watumiaji wengi wamekuwa wakilalamikia mabadiliko hayo yaliyofanywa siku za hivi karibuni. Ukitazama maoni ya watumiaji kwenye App Store na Google Play utaona malalamiko mengi ni kwa sababu ya mabadiliko ya muonekano. Baadhi ya watu wanakusanya sahihi milioni 1.2 za watumiaji kwenye  Change.org wakiomba SnapChat warudishe muonekano wa mwanzo.

Kujibu malalamiko hayo, Snap Inc. ambao ndio wanaosimamia mtandao huo wa kijamii walisema; “Tunaelewa sana mabadiliko haya mapya ya Snapchat hayakuwafurahisha wengi”

“Kwa kuweka kila kitu kuhusu marafiki zako pamoja, lengo letu ni kukufanyia urahisi kuungana na wale uwapendao”

Wakaongeza kuwa: “Msingi huu mpya ni mwanzo tu, tutaendelea kuwasikiliza kwa ukaribu na kutafuta njia mpya kufanya huduma zetu kuwa bora kwa kila mmoja”

Hata hivyo mwanadada Kylie Jenner baadae aliandika tweet ingine siku iyo iyo akisisitiza kuwa hata hivyo bado anaipenda na ataendelea kuipenda SnapChat

still love you tho snap … my first love

— Kylie Jenner (@KylieJenner) February 21, 2018

Endelea kuwa nasi kwa kutufuata kwenye mitandao ya kijamii, na usisahau ku subscribu ili uwe wa kwanza kupata Habari, Uchambuzi na Makala mbali mbali z kisayansi na teknolojia. Pia usisahau ku acha maoni yako hapo chini na unaweza kuwasiliana nasi kwa barua pepe [email protected]

KWENYE Kylie Jenner, SnapChat
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?