MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Twitter ina mpango wa kuruhusu mtu yeyote kuwa verified
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Habari > Twitter ina mpango wa kuruhusu mtu yeyote kuwa verified

Twitter ina mpango wa kuruhusu mtu yeyote kuwa verified

Imeandikwa na Emmanuel Tadayo Miaka 5 iliyopita
Sambaza
Twitter ina mpango wa kuruhusu mtu yeyote kuwa verified

Akizungumza kupitia huduma ya Twitter ya Periscope Livestream, bwana Jack Dorsey ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Twitter amesema kwamba wako mbioni kuruhusu watumiaji wote wa mtandao huo wa kijamii kupata huduma hiyo ya kuthibitishwa.

Hapo awali, Twitter walipotambulisha huduma huu maarufu kama “alama ya bluu” ilikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuonyesha taarifa au maelezo yaliyothibitishwa tu, ambapo alama ya bluu ilitolewa kwa akaunti za watu mashuhuri na wenye ushawishi katika jamii kama vile Wasanii, Viongozi, Wanaharakati, Waandishi, Taasisi & Jumuiya na n.k.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Starlink kuanza kutoa huduma za intaneti Tanzania robo ya kwanza 2023

Mwaka 2016 Twitter waliruhusu mtu yeyote kuomba akaunti zao kuthibitishwa, ila Twitter ilihitaji watumiaji hao kutoa sababu za msingi kwa nini wanahitaji akaunti zao kuthibitishwa. Ili mradi wawe waandishi, wabunifu au watu wakubwa wenye ushawishi, ndo maana watumiaji wa kawaida wa Twitter mara nyingi maombi yao ya kuthibishwa hayakufaulu.

Nia yetu ni kufungua uthibitisho kwa kila mtu

”Nia yetu ni kufungua uthibitisho kwa kila mtu,” anasema Dorsey. ”Na kufanya hivyo kwa njia inayoweza kutenga ambapo watu wanaweza kuthibitisha ukweli zaidi kuhusu wao wenyewe na hatupaswi kuwa hakimu au kuwa na ubaguzi wowote kwa upande wetu.”

Dorsey hakufafanua zaidi huo mchakato wa kuthibitisha akaunti za watumiaji utakavyokuwa, ila jumuiya nyingine za mtandao kama vile Airbnb akaunti yako ili iweze kuthibitishwa zinahitaji watumiaji wake kuwasilisha akaunti zao za facebook, namba za simu, anwani ya barua pepe au ID ya picha iliyotolewa na serikali.

WATUMIAJI WANADHANI WANAPOTHIBITISHWA NI KAMA WAMEAMINIWA, KUMBE SIO TUNAVYOAMAANISHA.

Dorsey anaongeza, kwamba kukujulikana na kutojulikana ni sehemu kitu muhimu sana kwa Twitter pia anasisitiza kwamba Twitter haimlazimishi mtu yeyote kuweka taarifa zake halisi kama jina, namba za simu bali tunataka iwe jukwaa ambalo mtumiaji atajisikia huru kulitumia  kuzungumza chochote alichonacho pasipo kuweka taarifa binafsi ambazo kwa namna moja au nyingine zinaweza kumuingiza kwenye matatizo. Pia ameongeza kwamba timu yao inafanya kazi kubwa kuzifuatilia kwa ukaribu akaunti wanazozitilia mashaka kuacha kutoa taarifa za uongo ikibidi kuzuia machapisho yao.

Viongozi wa Twitter kuzungumza live kupitia periscope ni moja kati taraibu walizojiwekea kuzungumza mafanikio na changamoto wanazopitia, mfano kwenye kikao hiki Dorsey alikutana na viongozi wengine wa Twitter kuzungumza masuala ya usalama ya watumiaji, na jinsi gani wanakabiliana na taarifa za uongo kwenye mtandao wao pia maudhui mabaya amabyo yapo kinyume cha sheria. Dorsey aliahidi kuwa makini na taarifa zisizo na ukweli kutochapishwa ingawa hakueleza ni njia gani watatumia.

”Tunakazi nyingi mbele yetu ambayo hatutaweza kuimaliza kwa usiku mmoja. Tutajitahidi kuwa mtandao ulio wazi kadri tuwezavyo.” alisema Dorsey.

Kitu hicho labda kinaweza kisiwe na chema sana kwetu na kinaweza kutuathiri sisi kwa njia nyingi ila tutajitahidi kufanya kila tuwezalo tuwe chombo kilicho wazi kwenu watumiaji na kuelezana  yote tunayokumbana nayo pamoja na changamoto zetu.

 

Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Wiki 1 iliyopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Wiki 2 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?