MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Facebook, WhatsApp, Instagram, na Messenger zapotea hewani
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Apps > Facebook, WhatsApp, Instagram, na Messenger zapotea hewani

Facebook, WhatsApp, Instagram, na Messenger zapotea hewani

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Mwaka 1 uliopita
Sambaza
Facebook, WhatsApp, Instagram, na Messenger zapotea hewani
Katika hali isiyo ya kawaida leo jumatatu tarehe 4, oktoba 2021 tovuti, app na huduma zingine za Facebook, WhatsApp, Instagram, na Messenger zapotea hewani. Mitandao hii mikubwa ya kijamii ambayo yote inamilikiwa na kampuni ya Facebook imetoweka kuanzia saa 12 jioni majira ya saa za afrika mashariki, ambapo watumiaji wengi duniani kote wamekumbwa na sintofahamu baada kushindwa kufikia huduma za mitandao hii.

Kwa mujibu wa tovuti ya DownDetector na taarifa kutoka ukurasa wa facebook twitter, tatizo hili limetokea saa kumi na mbili na dakika 44 (saa za afrika mashariki), na limewaathiri watumiaji dunia nzima. Kufikia saa moja jioni watumiaji zaidi ya 50,000 waliripoti kukumbwa na tatizo hili.

Mitandao yote mitatu ambayo ni mali ya Facebook, inaendeshwa kwa kutumia miundombinu ya pamoja ambapo huduma zingine zinazomilikiwa na Facebook kama vile Facebook Workplace na tovuti ya Oculus pia nazo zimepotea hewani.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Kupitia Twitter, Mkuu wa mawasiliano Facebook bwana Andy Stone aliandika kuwa wanaelewa kuwa kuna watu wanapata changamoto kufikia huduma za mitandao hiyo na wanalifanyia kazi hilo ili huduma ziendelee kama kawaida. Pia ujumbe unaofanana na huo umeandikwa kwenye kurasa za instagram na whatsapp hukohuko Twitter.

We’re aware that some people are having trouble accessing Facebook app. We’re working to get things back to normal as quickly as possible, and we apologize for any inconvenience.

— Facebook App (@facebookapp) October 4, 2021

Hii sio mara ya kwanza kwa mitandao hii inayomilikiwa na Facebook kupotea hewani mwaka huu, imetokea mara kadhaa ambapo tukio kubwa lilitokea mwezi wa nne, na lingine lilitokea mwezi wa sita 2021 ambapo inawezekana ndio kubwa zaidi kutokea ambapo instagram ilipotea hewani kwa zaidi ya masaa 16

Waswahili wanasema kufa kufaana, mitandao mingine ya kijamii ikiwemo Telegram na Signal imewakaribisha watumiaji wapya kuhamia kwenye mitandao hiyo wakisisitiza hakuna kupotea potea kwa huduma.

Pia kumeibuka meme mbalimbali zenye kuhusiana na tukio hili la kupotea kwa mitandao hii ya kijamii.

Instagram, facebook ,WhatsApp down. So I come to twitter and telegram😂 #facebookdown pic.twitter.com/n01IYiy5Nb

— JK’s_official_gf (ทานตะวัน🌻) (@JeonAnnA14) October 4, 2021

Muendelezo
Facebook yarudi hewani, pamoja na mitandao mingine ikiwemo Instagram na whatsapp.

Imejulikana tatizo lililoikumba Facebook mpaka kupotea ni matatizo ya DNS kwenye seva zake, hata hivyo tatizo hilo limetatuliwa na tayari mitandao hiyo imeanza kupatikana ena.

Kutokana na kupotea huko, mtandao wa Twitter nao mara kadhaa umeonekana kupotea, hii inasemekana ni kwa sababu ya kuzidiwa watumiaji kwani kwa mujibu wa taarifa Twitter imepata watumiaji wengi kupita wakati wowote ambao wamefungua mtanado huo kwa wakati mmoja tangu Twitter kuanzishwa.

  • Endelea kutembelea tovuti yetu ya Mtaawasaba ili tukujuze habari motomoto za teknolojia kila zinapotoka. Pia usisahau kutufollow twitter kupitia @Mtaawasaba na YouTube channel yetu.

KWENYE Facebook, Facebook Messenger, Instagram
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?