MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Google yazindua kituo cha kwanza cha maendeleo ya bidhaa barani Afrika
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Featured > Google yazindua kituo cha kwanza cha maendeleo ya bidhaa barani Afrika

Google yazindua kituo cha kwanza cha maendeleo ya bidhaa barani Afrika

Imeandikwa na Alice Kimathi Miezi 11 iliyopita
Sambaza
Google yazindua kituo cha kwanza cha maendeleo barani Afrika
Kampuni kubwa ya teknolojia ya Google yazindua kituo cha kwanza cha maendeleo ya bidhaa barani Afrika katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Kituo hiki cha maendeleo ya bidhaa kilichozinduliwa leo ni cha kwanza cha kampuni hiyo kuzinduliwa katika bara la Afrika.

Kituo hiki kipya cha maendeleo ya bidhaa kitasaidia kuunda bidhaa na huduma zitakazoleta mabadiliko kwa watu wa Afrika na duniani kote. Tayari, Google imetangaza fursa kwa watu zaidi ya 100 wenye vipaji katika uwanja wa teknolojia katika kipindi cha miaka 2 ijayo ili kusaidia kutatua changamoto ngumu na za kiufundi. Fursa hizi zitawahusu wahandisi wa programu, mameneja wa bidhaa, wabunifu wa UX na watafiti ili kuweka msingi wa ukuaji wa kituo hicho katika miaka ijayo.

Tangazo hili linakuja miezi 7 baada ya kampuni hiyo kuahidi kuwekeza dola za kimarekani bilioni 1 barani Afrika katika kipindi cha miaka mitano ijayo katika hafla yake ya Google for Africa mwezi Oktoba mwaka jana. Katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Sundar Pichai alisema watawekeza katika miradi ambayo itasaidia kuleta ukuaji wa teknolojia barani Afrika.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Tangu wakati huo imefungua kituo cha utafiti cha Google AI huko Accra, Ghana kusaidia kuendesha ubunifu. Mwezi uliopita, pia ilitangaza kuwa Equiano, kebo yake ya mtandao wa subsea, itawasili Togo, kisha Afrika Kusini, Namibia, Nigeria na St Helena zitafuata.

Google inatabiri kuwa Afrika itakuwa na watumiaji wa intaneti milioni 800 na theluthi moja ya idadi ya watu walio chini ya umri wa miaka 35 ifikapo mwaka 2030, na inataka kuwa mstari wa mbele katika harakati hii kwa kufanya kazi na “watu wenye nguvu, ubunifu, na ushirikiano ambao wanaweza kusaidia kutatua changamoto ngumu na muhimu za kiufundi, kama vile kuboresha uzoefu wa smartphone kwa watu barani Afrika”.

Google sasa imejiunga na orodha inayoongezeka ya makampuni makubwa ya teknolojia kama Microsoft na Visa ambayo yamezindua utafiti na maendeleo, na vituo vya uvumbuzi huko Nairobi, Kenya, kwa mtiririko huo.

Kama unahisi una kipaji, uzoefu, na uko tayari kufanya kazi na Google barani Afrika, unaweza kubofya hapa ili kuona fursa mbalimbali zilizotangazwa na Google.

KWENYE Google, kenya
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?