MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Vitu vya kuzingatia unapotaka kununua simu ya iPhone iliyotumika (2021)
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Mengineyo > Muongozo wa mtumiaji > Vitu vya kuzingatia unapotaka kununua simu ya iPhone iliyotumika (2021)

Vitu vya kuzingatia unapotaka kununua simu ya iPhone iliyotumika (2021)

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 7 iliyopita
Sambaza
zingatia haya kabla ya kununua iphone iliyotumika
Yaliyomo
Refurbished iPhoneUsed iPhoneMaduka yanayouza simuMaduka ya mtandaoniMkononiHitimisho
Unahitajika umakini wa hali ya juu unapotaka kununua simu ya iPhone iliyotumika, kwani waswahili wanasema ukizubaa unaachwa feri.

Simu za iPhone zimekuwa maarufu sana miaka ya karibuni, na iPhone 13 ni moja ya simu bora kabisa kuachiliwa mwaka 2021. Bei ya Simu hizi uwa imechangamka iwe unataka kununua mpya au unataka ku upgrade kutoka toleo la nyuma.

Kama lengo lako ni kununua simu nzuri ya iPhone bila kutoboa mfuko, basi njia rahisi uwa ni kununua iliyotumika. Changamoto kubwa inayokuja kwa kununua simu ya iPhone iliyotumika ni ubora wa bidhaa unayonunua vs bei utakayolipia, sio hivyo tu, pia hakuna garantii iyo simu itakuwa nzima kwa muda gani tofauti na simu mpya ambazo mara nyingi bei zake zinakuwa zinafanana na hata una uhakika wapi pa kuanzia ikitokea hitilafu yoyote unapoanza kuitumia simu yako.

Unaweza Kusoma

WWDC 2022: MacBook Air yenye Chip ya Apple M2 Yatangazwa

iOS 16 Imezinduliwa kwenye WWDC 2022

iPhone 15 hatimaye inaweza kuja na chaja ya USB-C

Kwa heri iPod. Apple yasitisha rasmi uzalishaji wa iPod

Aina ya simu zilizotumika

Kabla hatujaenda mbali zaidi, kwanza kabisa tujue aina ya simu zilizotumika. Kiufupi uwa kuna aina mbili ya simu zilizotumika.
  • Refurbished iPhone

ukisikia iPhone refurbished basi ujue ilirudishwa kwa Apple Store kufanyiwa marekebisho ili iwe katika viwango vinavyokubalika kuuzwa. Refurbished iPhone inaweza kuwa ni mpya ila ilipata hitilafu ndogo (mfano ikachubuka au ikapasuka kioo) au iliyotumika. Simu ambazo ni refurbished uwa zinakuja na waranti.
  • Used iPhone

hii ni iPhone iliyotumika na inauzwa kama ilivyo, sana sana uwa inakuwa wamei reset software. Kama ilikuwa na kioo kimepasuka au touch/face ID ina shida basi inauzwa hivyohivyo. Na mara nyingi wauzaji uwa wanasema kwa wateja changamoto ambazo simu hiyo inazo.

Nshawahi kununua simu kadhaa zilizotumika na hazikuwahi kunisumbua

Unaposikia neno “Simu iliyotumika” kitu cha kwanza kinachokuijia kichwani ni “itakuwa ni simu mbovu” au “imemshinda kuitumia anataka amsukumie mtu”. Inawezekana kuna ukweli ila sio lazima iwe hivyo kila wakati. Nshawahi kununua simu kadhaa zilizotumika na hazikuwahi kunisumbua.

Usipokuwa makini mara nyingi unaweza kuuziwa simu mbovu au yenye hitilafu kubwa ambayo gharama za matengenezo zinaweza kutosha kununua simu ingine. Sikatai nshawahi kukutana na bidhaa za namna hiyo pia. Sema kwa sababu najua najua kuhusu simu nagundua mapema na kupotezea.

Leo nimeamua kuandika miongozo hii angalau isaidie katika mchakato wa manunuzi ya simu zilizotumika, mchakato huu unaweza kufaa kuzingatia hata kwa bidhaa zingine kama tableti na kadhalika. Bila kupoteza muda tuanze kuangalia kipengele kimoja baada ya kingine.

Wapi unaweza nunua iPhone iliyotumika?

kuna njia au mahali tatu za kuweza kupata simu za iPhone zilizotumika, sehemu hizo ni pamoja na;

Maduka yanayouza simu

Kama uko dar es salaam, basi kuna maduka mengi yanayojulikana kwa kuuza simu zilizotumika, kuanzia makumbusho, kinondoni mpaka kariakoo. Tembelea maeneo hayo ili uweze jipatia simu. Kwa mikoani mnaweza tuandikia kwenye comment.

Maduka ya mtandaoni

Hapa ukiingia mitandao ya kijamii ya facebook, instagram au Twitter basi utakutana na maduka au watu wanaouza simu zilizotumika. Pia unaweza tembelea tovuti zinazohusika na kuuza bidhaa mbalimbali kama kupatana, Zoom Tanzania, na Tunzaa n.k.

Mkononi

Hii ni njia ingine ambayo unaweza nunua simu yako, kupitia kwa mtu unayefahamiana na e au lah anayeuza simu yake ya zamani.

 

 

 

 

 

 

Hitimisho

Kama utachukua muda, na umakini katika kununua simu ya iPhone iliyotumika unaweza pata simu nzuri na kwa gharama inayoendana nayo.

Pia, zingatia kwamba unaponunua simu iliyotumika uwa hakuna garantii itafanya kazi kama inavotarajiwa, ilo lisikuogopeshe maana najua waty kibao ambao wamenunua iPhone zilizotumika na hawajapata shida nazo japo wapo ambao wamepigwa na ndio maana tumekupa muongozo huu ili kukusaidia usipigwe na wewe.

Kuna lolote nimeliacha? Basi tuandikie kwenye comment hapo chini.

KWENYE Apple, iphone
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita
Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Miezi 4 iliyopita
Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Miezi 4 iliyopita
Apple inakabiliwa na kesi ya kukusanya taarifa kwenye simu za iPhone bila idhini

Apple inakabiliwa na kesi ya kukusanya taarifa kwenye simu za iPhone bila idhini

Miezi 4 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?