MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Simu
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Microsoft wazindua Windows 11 yenye muonekano tofauti kidogo na uliozoeleka
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • kompyuta
  • Maujanja
  • Apps
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Makala
    • Apps
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Matukio
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
    • Utamaduni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • intaneti
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • vifurushi visivyo rasmi
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Featured > Microsoft wazindua Windows 11 yenye muonekano tofauti kidogo na uliozoeleka

Microsoft wazindua Windows 11 yenye muonekano tofauti kidogo na uliozoeleka

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Mwaka 1 uliopita
Sambaza
Microsoft wazindua Windows 11
Leo jumanne tarehe 5, kupitia tovuti yao Microsoft wazindua Windows 11, toleo jipya kabisa la mfumo endeshi maarufu zaidi kwenye kompyuta wa Windows. Toleo hili linakuja kama maboresho ya bure kabisa kwa watumiaji wa mfumo endeshi tangulizi wa Windows 10.

ili uweze kuipata Windows 11, itakubidi usubiri mpaka pale kompyuta yako itakapokupa ujumbe wa ku update kupitia Windows Update. Hii itatokea kwa wale wenye kompyuta ambazo zina vigezo vinavyohitajika kuendesha mfumo huu wa Windows 11 tu, na ujumbe utaanza kuonekana majuma kadhaa yajayo baada ya leo.

Njia nyingine ambayo ni rahisi, ni kudownload na setup ya Windows 11 kupitia tovuti ya Microsoft halafu uiweke kwenye flash drive au DVD, kisha kuinstall mwenyewe kwa wakati wako na kwa utulivu.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Mabadiliko ambayo utakutana nayo mara tu utakapoanza kutumia Windows 11
Start menu iko katikati

kwanza kabisa utakutana na Start menu ikiwa katikati ya taskbar ambapo itakuwa na vitufe vingine, ambapo ukiibonyeza itakuletea orodha ya app unazozitumia mara kwa mara, hata hivyo ili kuepuka dhahama ya kubadilisha kabisa muonekano waliouzoea watumiaji, Windows 11 itakuruhusu kurudisha start button upande wa kushoto ulipozoeleka kupitia kwenye settings.

Mabadiliko kwenye muonekano

kama ni mtumiaji mzoefu wa mfumo endeshi wa Windows, basi utagundua mabadiliko hayo ya muonekano kuanzia kwenye vitufe mpaka mipangilio imekuwa ya kuvutia zaidi kuliko mwanzo.

Maboresho kwa watumiaji wa Touchscreen

Watumiaji wa touch screen wameboreshewa zaidi kwani sasaivi mfumo wa Windows 11 unafanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu kwa watumiaji wanaotumia kompyuta zenye kalamu maalumu (stylus).

Mabadiliko kwenye Windows Store

Windows Store imebadilishwa na kuwa Microsoft Store, moja ya maboresho makubwa ni upatikanaji wa app za android kupitia mfumo huu. Sasa ukienda Microsoft store na ukaandika “android apps” utaletewa Amazon App Store ambayo ukiinstall itakuwezesha kudownload na kuinstall apps za Android.

Hitimisho

sio watumiaji wote wataweza kupata toleo hili hasa watumiaji wa kompyuta za zamani kidogo. Kama kompyuta yako ni ya zamani unaweza kubaki na Windows 10 au unakunua kompyuta mpya.

 

KWENYE Microsoft, Windows 11
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Siku 4 zilizopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Siku 5 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?