MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Samsung Experience 9.0 yaja na maboresho ya Emoji
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Habari > Samsung Experience 9.0 yaja na maboresho ya Emoji

Samsung Experience 9.0 yaja na maboresho ya Emoji

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 5 iliyopita
Sambaza
Samsung Experience 9.0 yaja na maboresho ya Emoji

Kutegemeana na aina ya simu unayotumia, utagundua kuwa kuna tofauti katika Emoji zinazopatikana, ni utaratibu wa kawaida kwa watengenezaji wa simu kutengeneza Emoji za kipekee ili kujitofautisha na simu pinzani. Kwa upande wa Samsung tunaweza kusema wametumia vibaya uhuru huu kwa kutengeneza Emoji za tofauti sana ambazo zimekuwa zikileta mkanganyiko mkubwa kwa watumiaji wa Emoji izo.

Hata hivyo, katika sasisho kubwa la Android Oreo  ambalo Samsung wameachia siku kadhaa zilizopita kuna mabadiliko kadhaa ambayo yamefanyika. Kwa kawaida Samsung na watengenezaji wa simu wengine hutoa matoleo ya Android yakiwa na muonekano wa kitofauti kwa kuongeza au kupunguza baadhi ya vitu kutoka kwenye toleo la stock Android.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Katika toleo hili jipya la Android, Samsung wametoa Samsung experience 9.0 (zamani ikiitwa TouchWiz) ambayo katika maboresho waliyoongeza ni marekebisho ya Emoji. Emoji nyingi kwenye simu za Samsung zimekuwa tofauti na simu zingine, na hivyo kuleta mkanganyiko kwa watumiaji. Mabadiliko hayo ya Emoji yameonekana katika Maktaba ya Emoji (mabadiliko kutoka Samsung Experience 8.5 kwenda Samsung Experience 9.0)

Mfano mzuri wa Emoji iliyokuwa ikileta utata ni ile ya “rolling eyes” ambayo uwa inaonesha mtu anaezungusha macho kama ishara ya kutofurahishwa au kutoridhika na jambo. Katika picha hapa chini utaona kwenye Samsung experience 8.5 emoji imezungusha macho lakini uso unaokana kama unatabasamu tofauti na Emoji inavoonekana na simu au huduma za makampuni mengine.

 

Samsung_Experience_9_0_Emojipedia_Comparison_Rolling_Eyes_1

Cha kuvutia zaidi, sio maboresho Emoji iyo ya “rolling eyes” tu yaliyofanyika, bali kuna maboresho mengine kama;

imp-emoji-840x298Samsung-Experience-9-0-Emojipedia-Comparison-Faces-Tilt-Removed-840x298samsung-drool-face-840x298grimace-emoji-840x298

Cha kupendeza zaidi ni mabadiliko ya muonekano wa Cookie ambapo mwanzo ilionekana kama biskuti

Samsung-Experience-9-0-Emojipedia-Cookie-1

Mwisho kabisa, kuna emoji mpya nyingi za kutosha zilizoongezwa kwenye Samsung Experience 9.0.  Unaweza kuangalia Emoji mpya zote hapa, japo kuna emoji nyingi pia mabazo hazijafanyiwa mabadiliko yoyote.

Emoji hizi mpya zitaanza kuonekana kwenye simu za Galaxy S8/S8+ ambazo zitapokea sasisho jipya la Android Oreo naSamsung Experience 9.0, na pia tunatarajia kuziona kwenye simu mpya ya Galaxy S9 ambayo tunatarajia itazinduliwa siku zijazo mwezi huu wa pili katika maonesho ya MWC 2018 huko Barcelona Hispania.

Endelea kuwa nasi na usiache kutufuatilia kwenye mitandao mbali mbali kijamii ili usipitwe na Habari, Uchambuzi na Makala mbali mbali za kiteknolojia. kwenye Facebook, Twitter, Instagram, Google+ na Youtube, Pia usisite kutoa maoni yako hapo chini au tuandikie barua pepe kwa [email protected]

Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Wiki 1 iliyopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Wiki 2 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?