MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Umoja wa nchi za Ulaya kulazimisha matumizi ya USB-C kwa simu zote, na vifaa vingine
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Habari > Umoja wa nchi za Ulaya kulazimisha matumizi ya USB-C kwa simu zote, na vifaa vingine

Umoja wa nchi za Ulaya kulazimisha matumizi ya USB-C kwa simu zote, na vifaa vingine

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 2 iliyopita
Sambaza
USB-C kwa simu zote
Yaliyomo
Apple hawajafurahishwa na sheria hiiNchi za Afrika zitaathirika?hitimisho
Kamisheni ya Ulaya, ambayo ndio msimamizi wa sheria wa umoja wa nchi za ulaya, umepitisha mswada ambao kama utapishwa utakuwa sheria itakayolazimisha matumizi ya chaja za USB-C kwa simu zote, makampuni yanayotengeneza simu na vifaa vingine vya kielektroniki yatatakiwa kutengeneza simu zenye port zenye kuingiza chaja za USB-C

Lengo la mswada huu ni kuondoa uchafuzi, na kufanya maisha ya watumiaji wa vifaa vya kielektroniki kuwa rahisi kwa kuruhusu chaja moja kutumika na vifaa tofauti zaidi ya kimoja.

Sheria hii itatumika kwenye vifaa vingine kama spika zinazobebeka, tableti, headphone, kamera na makampuni yatatakiwa kutumia viwango vya chaja vitakavyokubalika na vifaa vyote. Hata ivyo sheria hii haigusi chaja ambazo ni wireless. Hii ni kwa sababu umoja wa ulaya wanaamini bado kuna ugunduzi mwingi kwenye eneo hilo.

Unaweza Kusoma

Elon Musk ametangaza rasmi vita na Apple

Ramani, kutoka Tanzania yakusanya $32m kurahisisha mnyororo wa usambazaji

Tovuti ya iCloud ya Apple yapata muonekano mpya, inavutia zaidi.

Starlink kuanza kutoa huduma za intaneti Tanzania robo ya kwanza 2023

Makampuni mengi ya vifaa vya kielektroniki hasa ya simu za android tayari wanatumia mfumo huu USB-C isipokuwa kampuni ya Apple kwenye simu za iPhone.

Apple hawajafurahishwa na sheria hii

Apple ambao wanatumia USB-C kwenye bidhaa zao kama MacBook na iPad, lakini kwenye simu za iPhone wanatumia chaja maarufu kama lightining chaja.Apple wamekuwa wakilalamikiwa sana kwa kuwanyima watumiaji wa iPhone fursa ya kutumia chaja zingine.

Lakini haya yanaweza kubadilika kufuatia mswada huu mpya. Apple wanaweza kulazimika kubadili na kuanza kutumia chaja za USB-C pia.

Msemaji wa Apple ameandika kuwa wao kama kampuni wanasimamia ubunifu na nini wateja wanataka. Na wanasimama na umoja wa ulaya katika kulinda mazingira. Akaongeza kusema, wanasikitishwa na uamuzi huu wa umoja wa ulaya kwani unazuia ubunifu, na pia utamiza watumiaji wa iPhone kwa nchi za ulaya maana tayari wana simu zenye chaja za lightining, na itakuwa uchafuzi wa mazingira kama watalazimika kuwa na zingine za Type-C.

Nchi za Afrika zitaathirika?

Ulaya inachukua sehemu kubwa ya mauzo kwenye soko la simu janja, kulazimisha kutumia viwango vinavyofanana kwa simu zote kwenye bara hilo hakutaacha salama sehemu zingine za dunia ikiwemo Afrika.

Ili kuondoa usumbufu kuna uwezekano mkubwa wa makampuni kuamua kutumia viwango vya kufanana dunia nzima.

Soko la simu janja hasa zile kwa ajili ya kawaida (midrange) na zile za hali ya juu kwa nchi za kiafrika linakuwa kwa kasi, ambazo ndizo zinazotumia USB-C, hivyo inawezekana kabisa mabadiliko kutokea kwa simu zote.

hitimisho

mswada huu ni sehemu ya mapitio ya mswada wa Radio Equipment Directive ambao utahitaji kupigiwa kura na bunge la ulaya ili kuwa sheria.

kama itapitshwa kuwa sheria, basi makampuni yanayotengeneza simu yatapewa miaka miwili kabla sheria hii haijaanza kuwabana.

Mwaka 2020 bunge la ulaya lilipiga kura kuwe na sheria mpya itakayotaka kuwa na chaja za kufanana kwenye simu na bidhaa zingine za kielektroniki.

KWENYE Apple
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Sasa unaweza pata Blue Tick kwa kulipia Instagram na Facebook

Wiki 1 iliyopita
Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Airtel yawa ya kwanza kuzindua huduma ya kadi za eSIM Tanzania

Wiki 2 zilizopita
Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Instagram yazindua Notes, Candid Stories, na Zaidi

Miezi 3 iliyopita
Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Umoja wa Ulaya waishinikiza Apple kuruhusu maduka mbadala ya programu kwenye iPhones na iPads

Miezi 3 iliyopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?