MtaawasabaMtaawasaba
  • Habari
  • Android
  • Kompyuta
  • Windows
  • Maujanja
  • StartUps
Mengineyo
  • Muongozo
  • Maujanja
  • Programu
  • Simu Janja
  • Teknolojia
Mtaawasaba
  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Mitandao
  • Facebook
  • Twitter
  • Instagram
  • YouTube
  • Newletters
© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive
Unasoma Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G
MtaawasabaMtaawasaba
  • Apple
  • Maujanja
  • StartUps
  • Magari
  • Mtaawasaba
    • Habari
    • Maujanja
    • Kompyuta
    • Simu Janja
    • Magari
    • Muongozo wa mtumiaji
    • Mitandao ya kijamii
    • Programu
    • Teknolojia
    • Mfumo endeshi
    • Miwani Janja
    • Saa Janja
    • Televisheni
  • Mengineyo
    • Microsoft
    • Windows
    • SnapChat
    • TTCL
    • Tigo Tanzania
    • Google
    • halotel
    • Instagram
    • iOS
  • Kuhusu Mtaawasaba
    • Kuhusu Sisi
    • Sera ya faragha
    • Vigezo na Masharti
    • Wasiliana Nasi
Una akaunti? Ingia
Tufuate mtandaoni
© 2022 Mtaawasaba Interactive. Haki zote zimehifadhiwa.
Mtaawasaba > Teknolojia > Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G

Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G

Imeandikwa na Alexander Nkwabi Miaka 10 iliyopita
Sambaza
Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G
Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G. Wateja wa Vodacom sasa wanauwezo wa kutumia teknolojia ya Long Term Evolution – LTE ambayo ni ya kisasa zaidi ulimwenguni katika utoaji wa huduma za Mawasiliano na hivyo kupunguza gharama katika kuwasiliana kufuatia kampuni hiyo kwa kushirikiana na Kampuni ya Nokia Siemens kuwawezesha wateja wake kufanya hivyo katika mradi wa majaribio unaohusisha eneo la Msasani jijini Dar es salaam.

Majaribio hayo yanafanywa kwa ushirikiano na kampuni ya Nokia Siemens yatahusisha eneo lote la Msasani jijini Dar es salaam kwa lengo la kuwawezesha wateja wa kampuni hiyo kuona ubora wa teknolojia hiyo katika kupokea huduma za simu za mkononi ikiwemo kupiga simu, kutumia huduma za Intaneti n.k

Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G

Unaweza Kusoma

WhatsApp inafanya majaribio ya malipo kwa sarafu za kidigitali

Jinsi ya Ku Activate Windows 11 Matoleo Yote Bure Bila Programu ya Ziada

Vodacom Tanzania waja na M-Pesa visacard

Microsoft wazindua Windows 11 yenye muonekano tofauti kidogo na uliozoeleka

Ni hatua nyingine muhimu kutoka Vodacom tunapowawezesha wateja wetu kupata kile ambacho ni wazi kitawapunguzia gharama katika matumizi ya huduma zetu sokoni bila ya kuwepo na mabadiliko ya gharama. “Alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Rene Meza wakati akitangaza rasmi kuanza kwa majaribio hayo leo jijini Dar es salaam LTE inayofahamika pia kwa jina la 4G ndio teknolojia ya kisasa zaidi ulimwenguni ambayo imedhihirisha uwezo wa hali ya juu katika mawasiliano ikiwemo huduma za intanteti katika kudadavua mitandao kupata filamu, machapisho, michezo ya kwenye kompyuta n.k

Kwetu sisi kuwawezesha wateja wetu kuweza kuijaribu teknolojia bora na ya kisasa zaidi ni kielelezo cha namna ambavyo Vodacom inavyoishi kimatendo kwa dira yake katika kuongoza mageuzi katika sekta ya huduma za simu za mkononi nchini.

Alisema Meza na kuongeza kuwa “Tunaona fahari kubwa namna kampuni yetu inavyokwenda sanjari na wimbi la mabadiliko ya teknolojia lililopo katika muktadha wa utandawazi, na namna inavyozitumia kwa ufasaha faida za kiteknolojia siku hadi siku katika kukidhi matakwa ya wateja wake.

Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G

Meza amesema Vodacom imeanza na Msasani kutokana na eneo hilo kuwa na uwiano mzuri wa shughuli za kibiashara na makazi ambazo zote zinahitaji huduma za Intaneti zenye kasi za kiwango cha LTE ingawa mipango ni kuisambaza teknolojia hiyo katika maeno mengine nchini “

Tunatambua kuwa njia za masafa ya hewa ya mawasiliano kwa mfumo wa LTE kwa sasa zimejaa hapa nchini hata hivyo bado Tanzania haijafikiwa kwa ukamilifu na huduma za Intaneti zenye kasi, hivyo basi ni matumaini yetu kwamba serikali itatupatia muongozo ili nasi kupitia mtandao mpana wa Vodacom tuwwawezeshe watanzania wengi zaidi kufikiwa na huduma za Teknohama zenye ubora unaoendana na mahiraji ya sasa.”

Vodacom Yaanza Majaribio Matumizi ya 4G

Kwa upande wake, Mkuu wa huduma za Vodacom katika kampuni ya Nokia Siemens Pete Beadle, alisema kiwango cha juu cha teknolojia za mawasiliano ndani ya kampuni hiyo duniani kote imekuwa ni chaguo la majaribio kwa kampuni zinazotoa huduma zinazozingatia teknolojia za kisasa, kutokana na dhana yake ya mwingiliano wa zaidi ya teknolojia moja na kwa lengo moja linalozingatia matakwa, kasi na viwango vya ubora.

Beadle, aliongeza kuwa kiuhalisia na kwa kuzingatia mahitaji ya soko nchini, Vodacom ndio kampuni pekee iliyojipanga kutoa huduma hiyo ya kasi kwa kuwa tayari. Hadi sasa imekwisha kamilisha awamu ya kwanza ya upitishaji wa huduma zake katika mkongo wa taifa wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (NICTBB) pamoja na ule wa mawasiliano wa baharini unaopita sehemu kubwa duniani.

@Mtaawasaba

KWENYE Vodacom Tanzania
Sambaza chapisho hili
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Telegram Barua Pepe Nakili kiungo Durufu
Acha Ujumbe

Toa Jibu Ghairi kujibu

Barua-pepe haitachapishwa. Fildi za lazima zimetiwa alama ya *

Mtaawasaba Newsletter

Jiunge nasi kwa njia ya barua pepe tukujulishe kila inapotoka habari mpya

Zaidi Kutoka Mtaawasaba

Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Teknolojia ya hali ya juu kutumika katika Kombe la Dunia la FIFA Qatar 2022

Miezi 4 iliyopita
Vodacom Tanzania imezindua huduma ya teknolojia ya 5G

Vodacom Tanzania imezindua huduma ya teknolojia ya 5G

Miezi 7 iliyopita
NALA yakusanya bilioni 23.1

Kampuni ya huduma za kifedha ya NALA yakusanya bilioni 23.1 za uwekezaji

Mwaka 1 uliopita
Simu zinazotumia Blackberry OS kuacha kufanya kazi kuanzia Januari 4

Simu zinazotumia Blackberry OS kuacha kufanya kazi kuanzia Januari 4

Mwaka 1 uliopita

© 2013 - 2023 Mtaawasaba Interactive. Crafted by Simba Creative

  • Kuhusu Sisi
  • Sera ya faragha
  • Vigezo na Masharti
  • Wasiliana Nasi
Go to mobile version
logo logo
Karibu Mtaawasaba!

Jaza taarifa kuingia Kwenye Akaunti Yako

Umesahau Nywila?